Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 193 2023-04-28

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: -

Je, lini mpaka wa Kasesya/Zombe utafanya kazi kwa ufanisi ili kupunguza msongamano wa malori katika mpaka wa Tunduma?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa mpaka wa Tunduma/Nakonde na mpaka wa Kasesya/Zombe ambayo inatumika kupitisha mizigo inayokwenda au kutoka Zambia. Aidha, wasafirishaji wana hiari ya kuchagua mpaka upi wautumie katika kusafirisha mizigo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka wa Tunduma/Nakonde umekuwa ukitumiwa zaidi na wasafirishaji wanaosafirisha mizigo kutoka Dar es Salaam kwenda Zambia na DRC kwa kuwa ndiyo mpaka wenye umbali mfupi ukilinganishwa na mpaka wa Kasesya/Zombe. Kwa mfano, kutoka Dar es Salaam hadi Tunduma ni kilomita 922, kutoka Dar es Salaam kwenda Kasesya kupitia Tunduma na Laela ni kilometa 1,172; kutoka Dar es Salaam kwenda Kasesya kupitia Tunduma na Sumbawanga ni Kilometa 1,249; na kutoka Dar es Salaam kwenda Kasesya kupitia Dodoma,Tabora na Mpanda ni Kilometa 1,530. Ahsante.