Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 192 2023-04-28

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa miundombinu chakavu katika Vyuo Vikuu?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantum Mzamili Zodo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua changamoto ya uchakavu wa miundombinu katika Vyuo Vikuu vya Umma hapa nchini. Ili kutatua changamoto ya uchakavu wa miundombinu vyuoni Serikali imefanya ukarabati wa miundombinu mbalimbali katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya na Chuo Kikuu cha Ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa sasa inaendelea na ukarabati wa miundombinu chakavu na ujenzi wa miundombinu mipya katika Vyuo Vikuu vyote vya Umma 14

na Taasisi tano (5) za Elimu ya Juu zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango ili kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji vyuoni. Aidha, Taasisi hizi zimekwishapokea fedha kwa ajili ya kuendelea na ukarabati na ujenzi wa miundombinu kupitia Mradi wa Mageuzi ya Uchumi katika Taasisi za Elimu ya Juu (HEET).

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.