Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 191 2023-04-28

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: -

Je, Serikali ipo tayari kuondoa kodi kwenye vifaa vinavyotumiwa na Watu wenye Ulemavu wakati wa kuingia nchini?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), SURA 148 na ushuru wa forodha kwenye vifaa vilivyotengenezwa mahsusi kwa ajili ya Watu Wenye Ulemavu. Msamaha wa VAT umeainishwa katika kipengele cha 8 na 12(d) cha Jedwali lililopo kwenye Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, Sura ya 148.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vifaa vilivyopewa msamaha wa kodi ni pamoja na baiskeli na magari yaliyotengenezwa mahususi kwa matumizi ya watu wenye ulemavu. Vile vile, Serikali imetoa msamaha wa VAT kwenye huduma za elimu zinazotolewa katika vituo vya mafunzo ya mwili na akili kwa watu wenye ulemavu, ahsante.