Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 190 2023-04-28

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kuupitia tena Muundo wa Utumishi wa Madaktari Bingwa wa mwaka 2022?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alice Karungi Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza Waraka wa Maendeleo ya Utumishi Na.1 wa mwaka 2009 kwa kada zilizo chini Wizara ya Afya ambao umeainisha miundo na sifa za wataalam mbalimbali wanaopaswa kuajiriwa na kufanya kazi katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inakamilisha Mapitio ya Miundo ya kada za afya ambayo inatarajiwa kukamilika Mwezi Mei, 2023 na kuwasilishwa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa ajili ya kupata idhini. Miundombinu hii itakapokamilika itaweza kukidhi mahitaji ya kiutumishi kwa wataalam mbalimbali wa afya wakiwemo Madaktari Bingwa.