Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 189 2023-04-28

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuiliza: -

Je, ni kesi ngapi za Wakulima kulishiwa mazao yao zimeripotiwa na ngapi zimepelekwa Mahakamani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jonas Van Zeeland, Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mashauri ya kesi za wakulima kulishiwa mazao yao zilizoripotiwa Vituo vya Polisi katika Wilaya ya Mvomero kuanzia Januari, 2022 hadi Machi, 2023, ni jumla ya Mashauri 343. Kesi zilizofikishwa mahakamani ni
184. Kati ya hizo kesi 119 zimehukumiwa, kesi 65 zinaendelea kusikilizwa mahakamani na kesi 159 zipo kwenye hatua mbalimbali za uchunguzi na upelelezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.