Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 187 2023-04-28

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: -

Je, mpango wa kutumia majengo ya Sekondari ya Sengerema kuwa Chuo cha Madini na Uvuvi umefikia wapi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tabasam Hamis Mwagao, Mbunge wa Jimbo la Sengerema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Sekondari Sengerema ni miongoni mwa shule za Sekondari kongwe hapa nchini. Shule hii inachuka wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha sita kutoka nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inapanga kuongeza nafasi kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha Tano na Sita, kutokana na wanafunzi wanao maliza kidato cha nne kuongezeka sana. Mpango wa kuifanya Shule ya Sekondari Sengerema kuwa Chuo cha Madini na Uvuvi hauwezekani kutokana na uhitaji wa shule hii kwani kubadili matumizi ya shule hii kutaongeza uhaba wa nafasi za wanafunzi wa kidato cha Tano na Sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Rais TAMISEMI haijashirikishwa kwa namna yoyote kuhusu kubadili matumizi ya shule ya Sekondari Sengerema. Hivyo, tunawaomba wenzetu wa Wizara ya Madini kuja mezani na kujadiliana juu ya jambo hili, hasa ikizingatiwa kuwa kwa sasa tuna uhitaji mkubwa wa shule za kidato cha tano na sita. Aidha tunaomba kuwashauri Wizara ya Madini kutafuta eneo na fedha kwa ajili ya kujenga chuo kitakachojihusisha na kada ya madini kuliko kubadili matumizi ya Sekondari hii.