Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 186 2023-04-28

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga shule ya Kidato cha Tano na Sita katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Idi Mpakate, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uhitaji wa shule za kidato cha tano na sita kwa maeneo mengi hapa nchini, Shule ya sekondari ya Mchoteka katika jimbo la Tunduru, wazazi pamoja na halmashauri walijenga hosteli mbili ambazo zimekamilika; hostel moja ipo katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshapeleka kiasi cha shilingi milioni 160 kwa ajili ya kuongeza miundombinu mingine ili kukidhi vigezo vya kupandisha hadhi shule. Hata hivyo, shule hii imeombewa usajili wa mkondo walau mmoja wa kidato cha tano.