Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 185 2023-04-28

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaongeza madarasa katika Shule ya Msingi Puma kutokana na kuzidiwa na idadi ya wanafunzi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kuwa kutokana na utekelezaji wa sera ya elimu bila ada, kumepelekea ongezeko kubwa la wanafunzi na uhitaji wa miundombinu ya shule ikiwemo madarasa. Hatua mbalimbali za kukabiliana na uhitaji wa miundombinu ya shule zinaendelea kufanywa na Serikali katika halmashauri, manispaa na majiji hapa nchini ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kukabiliana na ongezeko kubwa la wanafunzi katika shule ya Msingi Puma, Katika bajeti ya mwaka 2023/2024 shule hii imetengewa madarasa mawili sambamba na ufunguzi wa shule shikizi Isalanda ambayo itasaidia pia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule ya msingi Puma.