Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 163 2023-04-25

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuwa na Sera ya kuongeza tija katika sekta ya kilimo kwenye Mikoa ya Kanda ya Kati?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Kilimo ya Taifa ya mwaka 2013, inatambua umuhimu wa kuongeza tija kwenye uzalishaji wa mazao ya kilimo. Kupitia sera hiyo, maeneo ya
kipaumbele ya kuongeza tija ni pamoja na kuimarisha utafiti, kuongeza upatikanaji wa pembejeo bora za kilimo (mbegu, mbolea na viuatilifu), kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji, kupima udongo, kuimarisha matumizi ya zana bora za kilimo na kuimarisha huduma za ugani katika kanda zote za Ikolojia nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza miradi ya umwagiliaji katika Mikoa ya Kanda ya Kati – Dodoma, Singida na Tabora kwa kujenga mabwawa saba na skimu za umwagiliaji kumi; uimarishwaji wa Vituo vya Utafiti vya Tumbi, Makutupora na Hombolo; usambazaji wa mbegu bora kwa wakulima; na uimarishwaji wa huduma za ugani ikiwa ni mkakati katika utekelezaji wa Sera ya Kilimo ya Taifa ya Mwaka 2013.