Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 84 2023-04-14

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Kibiti?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana na kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu nikiwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria nimshukuru Mwenyezi Mungu lakini pia nimshukuru Mheshimiwa Rais kuendelea kuniamini naahidi kwamba nitaendelea kufanya kazi kwa unyenyekevu mkubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria sasa naomba kujibu swali Mheshimiwa Twaha Ally kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mahakama inaendelea kutekeleza mpango wake wa ujenzi na ukarabati wa majengo katika ngazi zote. Katika mpango huo, Mahakama ya Wilaya ya Kibiti imepangwa kujengwa katika mwaka wa fedha 2023/2024. Aidha, maandalizi ya awali yameshaanza kufanyiwa kazi na kukamilika, ikiwemo usanifu wa mradi, pamoja na maandalizi ya kabrasha za zabuni. Hivyo, mara baada ya bajeti kuanza, utekelezaji wa mradi huu utaanza mara moja. Ahsante.