Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 65 2023-04-12

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI K.n.y. MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga chujio la kuchuja na kutibu maji toka chanzo cha maji Nyamtukuza kabla ya kuyapeleka kwa wananchi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Nyangh’wale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali Serikali ilipanga kujenga chujio la maji kwenye chanzo cha maji cha Nyamtukuza kwa ajili ya kuwapatia huduma ya maji safi na salama wananchi wa vijiji vya Nyangh’wale. Hata hivyo, kwa kuwa bomba kuu la KASHWASA linapita karibu, Serikali ilifanya usanifu wa kuchukua maji eneo la Mhangu na kubaini unafuu wa gharama ikilinganishwa na ujenzi wa chujio hivyo ilijenga mradi kupitia bomba hilo na hadi sasa vijiji 21 vinanufaika. Maji ya KASHWASA tayari yametibiwa na ni safi na salama na yatatosheleza mahitaji ya maji kwa wananchi wa Nyangh’wale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa chujio sasa zinatumika kujenga miundombinu ya kusambaza maji kwenye vijiji vya Nyaruguguna, Nyamgogwa, Iseni, Nyangalamila, Kabiga, Nwiga, Bukungu, Bumanda, Kanegere, Mimbili na Isonda. Serikali itajenga chujio la kuchuja na kutibu maji Nyamtukuza kulingana na mahitaji ya huko baadaye.