Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 59 2023-04-12

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti matukio ya ubakaji na ulawiti katika shule za bweni?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda sasa kujibu swali la Mheshimiwa Kabula Enock Shitobela Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama sehemu ya kudhibiti matukio ya ubakaji na ulawiti kwa wanafunzi, Serikali imetoa Waraka wa Elimu namba 11 wa mwaka 2002 kuhusu malezi, unasihi na ulinzi wa mtoto ambapo Waraka unaelekeza kila shule na chuo cha ualimu kuanzisha huduma za malezi na ushauri nasaha kwa wanafunzi. Katika utekelezaji wa Waraka huo Serikali imewezesha mafunzo kwa walimu wawili wa ushauri na unasihi kwa kila shule pamoja na kuanzisha dawati la ulinzi na usalama wa mtoto shuleni kwa lengo la kutoa fursa kwa wanafunzi kuzungumza na kuripoti vitendo vya unyanyasaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia imetoa Waraka wa Elimu namba mbili wa mwaka 2023 kuhusu utoaji wa huduma ya bweni kwa wanafunzi wa elimu ya awali na msingi ambapo waraka huu unaelekeza kuwa huduma ya bweni itolewe kwa wanafunzi kuanzia darasa la tano na kuendelea. Hatua hii imezingatia ukweli kuwa wanafunzi wa umri huo walau wana upeo wa kutambua baya na zuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wito wangu kwa wazazi, walezi na jamii kwa ujumla ni kushiriki kikamilifu katika ulinzi wa mtoto dhidi ya vitendo vya unyanyasaji wawapo shuleni na majumbani pia.