Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 49 2023-04-11

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza kulipa fidia Wananchi wa Makole waliopisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege na Mkonze waliopisha ujenzi wa SGR?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Yusuph Majalla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania (TAA) imekamilisha malipo ya fidia kwa wananchi kutoka kaya 14 za Mtaa wa Chaduru B, Kata ya Makole, Dodoma Mjini, zilizopisha upanuzi wa Kiwanja cha Ndege Dodoma. Fidia hiyo, iligharimu kiasi cha shilingi 1,900,000,000, ilihusu upanuzi wa kiwanja kwa mita 150 zilizohitajika. Serikali haitahitaji kupanua zaidi Kiwanja cha Ndege cha Dodoma kwa kuwa imeanza kujenga Kiwanja cha Ndege cha Msalato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) imekamilisha tathmini ya fedia kwa wananchi wote wa Mkonze ambao maeneo yao yatatwaliwa kwa ajili ya ujenzi wa SGR. Zoezi la ulipaji wa fidia lilianza kufanyika kuanzia tarehe 4 Aprili, mwaka huu 2023. Naomba wananchi ambao bado hawajalipwa wawe na subira wakati zoezi la malipo likiendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, naomba kuwafahamisha Waheshimiwa Wabunge kuwa, ujenzi wa reli ya SGR unafanyika kwa utaratibu wa Sanifu na Jenga (Design and Build), hivyo utwaaji wa maeneo ya nyongeza utaendelea kufanyika kwa kadiri ya mahitaji, kwa mujibu wa sheria, na taratibu za nchi, ahsante.