Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 45 2023-04-11

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme katika Vijiji Nane vya Wilaya ya Mufindi ambavyo havijapata umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nancy Hassan Nyalusi, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mufindi ina jumla ya vijiji kumi tu ambavyo havina umeme na vinapatiwa umeme kupitia Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili, kupitia Mkandarasi anayeitwa OK Electrical Services Limited. Hadi kufikia mwezi Aprili, 2023 vijiji vinane vilikuwa vimeshapatiwa umeme na vijiji viwili (2) vijulikanavyo kwa majina ya Itika na Mpangatazara bado havijapatiwa umeme. Vijiji vyote vinatarajiwa kupatiwa umeme ifikapo mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.