Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 44 2023-04-11

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua vituo vingi zaidi vya kuuza gesi asilia?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiachana na usambazaji wa gesi asilia kwa kutumia bomba la kusafirisha gesi Mtwara, Lindi, Pwani na Dar es Salaam, kuna vituo vitatu vya kugandamiza na kuuza gesi asilia nchini (Compressed Natural Gas (CNG) Stations) ambapo Dar es Salaam viko viwili (2) na Mtwara kipo kimoja (1). Vituo viwili vinamilikiwa na wawekezaji binafsi na kimoja ni ubia wa Serikali na Sekta Binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2022/2023, Serikali imempata Mkandarasi wa ujenzi wa vituo vitatu (3) vya (CNG) na kazi hiyo itaanza kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha. Vilevile, kituo kimoja (1) kitajengwa na mwekezaji binafsi (Dangote) eneo la Mkuranga, Pwani. Aidha, Serikali imeshatoa idhini kwa kampuni binafsi 20 kujenga vituo vya kujaza gesi katika magari. Kampuni hizo zipo katika hatua mbalimbali za kupata vibali vya ujenzi.

Mheshimiwa Spika, katika hatua nyingine, Serikali imepanga kujenga vituo vya CNG katika Bohari Kuu za Serikali za Dar es Salaam na Dodoma ili kuwezesha magari ya Serikali na watu binafsi yanayoendelea kuunganishwa na mfumo wa kutumia gesi asilia kuweza kupata nishati hiyo. Taratibu za utekelezaji wa mradi huu zinakamilishwa Serikalini ili utekelezaji uanze mara moja.