Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 42 2023-04-11

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukabiliana na kupanda kwa bei za pembejeo za kilimo ikiwemo mbolea?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza Mbunge wa Mbeya Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepanga mikakati ya muda mfupi, kati na ya muda mrefu katika kukabiliana na kupanda kwa bei za mbolea hapa nchini. Mikakati hiyo ni pamoja na kutekeleza Mpango wa Utoaji Ruzuku ya Mbolea kwa wakulima msimu wa 2022/2023, kuhimiza matumizi ya mbolea mbadala wa DAP na UREA kama vile NPK, NPS, NPS- zinc, Minjingu, mbolea za asili na chokaa, kupunguza gharama za meli kukaa bandarini ambazo pengine mwisho wake hujumuishwa kwenye mjengeko wa bei ya mbolea, kuhimiza wafanyabiashara wa mbolea kutumia njia ya reli ya TAZARA na Reli ya Kati kusafirisha mbolea kwa wingi kwenda mikoani na kuhamasisha uwekezaji katika kuzalisha mbolea ndani ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kupitia mpango wa ruzuku ya mbolea, Serikali imeweka bei elekezi ili kuwawezesha wakulima kununua mbolea za DAP, Urea na NPK kwa Shilingi 70,000 kwa mfuko wa kilo 50, Shilingi 60,000 kwa mfuko wa kilo 50 wa mbolea ya CAN na Shilingi 50,000 kwa mfuko wa kilo 50 wa mbolea ya SA. Aidha, Serikali inaendelea kushirikiana na Sekta Binafsi vikiwemo viwanda vya Minjingu Mines and Fertilizer Limited na Itracom Fertilizers Limited kuhakikisha uzalishaji na upatikanaji wa mbolea hapa nchini kwa gharama nafuu unaimarika na kupunguza utegemezi wa kuagiza mbolea kutoka nje ya nchi.