Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 3 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 35 2023-04-06

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: -

Je, kuruhusu Benki kuwa Wakala wa Bima Serikali haioni kuwa Mawakala wengine watafunga biashara kwa kukosa wateja?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na wadau wa bima ilianzisha BenkiWakala wa Bima ili kuongeza wigo wa usambazaji na upatikanaji wa huduma za bima kwa wananchi. Idadi ya Mawakala wa Bima wa Kawaida imekuwa ikiongezeka sambamba na BenkiWakala wa Bima kwa sababu hali hii imechochea ushindani, ubunifu na kutegemeana. Takwimu zinaonesha BenkiWakala waliosajiliwa kwa mwaka 2020 wako 14; mwaka 2021 wako 23; mwaka 2022 wako 27; na hadi 30 Machi, 2023 walishafika 30. Aidha, Mawakala wa Bima wa Kawaida waliosajiliwa kwa mwaka 2020 walikuwa 745; mwaka 2021 walikuwa 789; mwaka 2022 walikuwa 910; na kwa mwaka 2023 hadi Machi, 2023 wameshafika 960.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa takwimu hizi, ni dhahiri kuwa Mfumo wa BenkiWakala wa Bima umesaidia kukuza biashara ya Bima hapa nchini.