Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 112 2023-02-08

Name

Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza magari ya kisasa ya zimamoto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Salim Mussa Omar, Mbunge wa Gando kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji imekamilisha hatua zote za mkopo wa Euro milioni 4.9 kutoka Nchini Austria kwa ajili ya ununuzi wa magari 12 ya kuzima moto. Kati ya magari yanayonunuliwa mawili ni ya ngazi (Turntable ladder) kwa ajili ya kuzima moto katika majengo marefu. Aidha, Jeshi la Zimamoto na Uokozi linatarajia kupata magari matatu ya kuzimia moto ambayo yalipatikana kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021 kutoka Shirika la Nyumbu Tanzania Automotive Technology Center (TATC).