Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 69 2022-04-19

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ukosefu wa magari na nyumba za Askari Polisi Kituo cha Polisi Nungwi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Simai Hassan Sadiki, Mbunge wa Nungwi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi Nungwi ni kituo cha Daraja C na kipo Mkoa wa Kaskazini Unguja. Pamoja na kufanya kazi mbalimbali za kipolisi, hushughulikia pia na kusimamia majukumu ya utalii.

Mheshimiwa Spika, Kituo hiki kinacho gari Na. PT. 3388, Toyota Landcruiser ambalo hutumika kwenye kazi za kila siku za polisi. Kutokana na udogo wa eneo la kituo, hakuna sehemu inayoweza kutosheleza kujenga nyumba za makazi ya askari polisi. Hivyo, Serikali inawashauri wadau wenye nyumba za kupangisha wapangishe askari wetu. Aidha, uongozi wa Mkoa Kaskazini Unguja unaombwa ushirikiane na uongozi wa jamii kupata eneo linalofaa kujenga nyumba za askari ili Serikali iingize ujenzi wa nyumba hizo katika mpango.