Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 33 2022-09-14

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya wakulima na wafugaji katika Jimbo la Mlimba?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa changamoto mbalimbali zinazosabisha migogoro ya matumizi ya ardhi ikiwemo hiyo ya wakulima na wafugaji. Serikali imechukua hatua mbalimbali kuhakikisha migogoro ya matumizi ya ardhi katika Mkoa wa Morogoro hususan Wilaya ya Kilombero inatatuliwa.

Mheshimiwa Spika, miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi na kumilikisha ardhi kupitia Mradi wa Kuwezesha Umilikishaji wa Ardhi (LTSP) ambapo jumla ya vijiji 58 viliandaliwa mipango ya matumizi ya ardhi na Hakimiliki za Kimila 150,006 zilisajiliwa. Kati ya vijiji hivyo 58, vijiji 32 vipo katika Halmashauri ya Mlimba ambapo jumla ya Hakimiliki za Kimila 41,797 zimesajiliwa na 30,699 zimechukuliwa na wananchi.

Mheshimiwa Spika, nasisitiza Serikali za Halmashauri kuhakikisha zinasimamia mipango ya matumizi ya ardhi iliyoandaliwa ili kupunguza uwezekano wa kuibuka au kuendelea kwa migogoro baina ya watumiaji wa ardhi.

Mheshimiwa Spika, hatua nyingine zilizochukuliwa na Serikali ni kudhibiti na kuimarisha mbinu za utatuzi wa migogoro kwa kutoa elimu kupitia mikutano ya wananchi kuhusu mipango ya matumizi ya ardhi iliyowekwa kwa pamoja, kutungwa kwa Kanuni za Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi na kuhimiza matumizi ya ardhi yenye tija.

Mheshimiwa Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Wizara kwa kushirikiana na Wizara nyingine za kisekta zitaendelea kudhibiti na kushughulikia migogoro na kuitafutia ufumbuzi iliyopo ili kuimarisha ustawi wa jamii baina ya wakulima na wafugaji. (Makofi)