Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 93 2021-09-08

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: -

Je, ni lini viongozi wa Kitaifa wataanza kutembelea nchi za nje mahsusi kwa ajili ya kutafuta masoko ya mazao hususan mpunga na mahindi?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ziara za Viongozi wa Kitaifa nje zimekuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, kisiasa na kiuchumi kati ya Tanzania na nchi rafiki. Kutokana na matunda yanayopatikana kupitia ziara za Viongozi wa Kitaifa, Wizara imeendelea kushauri Mamlaka kutembelea nchi za kimkakati kwa kuzingatia maslahi ya Tanzania katika nchi husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, viongozi wetu wa Kitaifa tayari wamefanya ziara katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na zile za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Ni katika muktadha huo, mwezi Mei, 2021, Wizara iliratibu ziara ya kikazi ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Kenya, ambapo pamoja na mambo mengine alifanikiwa kutanzua, vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiforodha (NTBs) vilivyokuwa vikiwakabili wafanyabiashara wakiwemo waliokuwa wakisafirisha mahindi kwenda Kenya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kenya ni miongoni mwa wanunuzi wakubwa zaidi wa mahindi ya Tanzania kutokana na sifa zake, ubora wake na bei yake nzuri. Hali kadhalika, Wizara pia iliratibu ziara ya Mheshimiwa Rais Samia nchini Burundi, Rwanda na Uganda, ambapo pamoja na mambo mengine, Mheshimiwa Rais alitumia fursa hiyo kutafuta pia masoko ya bidhaa za mazao kutoka Tanzania ikiwemo mahindi, mpunga na maharage. Aidha, katika ziara ya Burundi, Mheshimiwa Rais aliongozana na ujumbe wa wafanyabiashara ambapo kulifanyika kongamano la biashara kwa lengo la kukuza wigo wa biashara kati ya Tanzania na Burundi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)