Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 54 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 449 2021-06-18

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Tanga – Mabokweni – Maramba – Daluni – Mtoni – Bombo – Magoma hadi Korogwe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Tanga – Mabokweni – Maramba – Daluni – Bombo Mtoni – Korogwe yenye urefu wa kilometa 127.69 ni barabara ya mkoa inayohudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS). Aidha, Sehemu ya barabara ya Tanga – Mabokweni yenye urefu wa kilometa 11.2 tayari imejengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kiuchumi wa barabara ya Tanga – Mabokweni – Maramba – Daluni – Bombo – Korogwe kwa wananchi wa maeneo ya Mashewa, Mabokweni, Maramba, Bombomtoni, Magoma na Daluni. Kwa kutambua umuhimu huo, Wizara imetenga fedha katika bajeti ya mwaka wa fedha ujao 2021/ 2022 kiasi cha shilingi milioni 1,275.4 ambayo ni sawa na bilioni 1.2754 ili kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii. Mara baada ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii. Aidha, barabara hii itaendelea kufanyiwa matengenezo mbalimbali ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Ahsante.