Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 417 2021-06-14

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:-

Je, ni lini Bandari ya Sota eneo la Shirati itaanza kurekebishwa ili kuinua uchumi, lakini pia kuboresha shughuli za kibiashara eneo la mpakani mwa Tanzania na Kenya?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Bandari ya Sota ni miongoni mwa Bandari za kati na ndogo 693 zilizoainishwa na Serikali kupitia Mamlaka ya Bandari (TPA) ili kutangazwa katika Gazeti la Serikali kwa lengo la kuzirasimisha. Aidha, mpango huo wa urasimishaji unakwenda sambamba na zoezi la kuhuisha Mpango Mkuu wa TPA wa kuendeleza Bandari zote nchini unaojumuisha Bandari ya Sota.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa mpango huo unafanyiwa mapitio na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, mwaka huu 2021. Baada ya mpango huo kukamilika, orodha ya bandari kwa ajili ya uendelezaji ikiwemo Bandari ya Sota eneo la Shirati itatolewa kwenye tangazo la Serikali ili zihuishwe, ahsante.