Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 33 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 278 2021-05-21

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kufuta madeni ya muda mrefu kwa wafanyabiashara wa ndani yatokanayo na ukosefu wa elimu juu ya matumizi sahihi ya mashine za EFD wanayodaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Henry Maganga, Mbunge wa Mbogwe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali ilitoa msamaha kwa wadaiwa wa kodi ili kuongeza makusanyo. Msamaha huu ulihusisha riba na adhabu zilizoambatana na madeni yote yaliyolimbikizwa kwa miaka ya nyuma. Msamaha huu ulilenga kusamehe malimbikizo ya nyuma ya riba na adhabu kwa kiwango cha asilimia 100 kwa wafanyabiasha wote hapa nchini ambao walikuwa na malimbikizo ya madeni ya kodi. Msamaha huo ulitolewa kwa kipindi cha miezi sita kilichoanzia tarehe 1 Julai, 2018 mpaka tarehe 31 Desemba, 2018 ambapo kutokana na kusuasua kwa utekelezaji wake, Serikali iliongeza muda wa msamaha huo kwa miezi sita ili wafanyabiashara waliokuwa na madeni hayo kuweza kukamilisha malipo husika yaliyotokana na msamaha huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua hiyo ya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi Sura 438 ilitarajiwa kuongeza mapato ya Serikali na kukusanya malimbikizo ya madeni ya nyuma ya kodi pamoja na kuinua kiwango cha ulipaji kodi kwa hiyari kwa zaidi ya asilimia 10.

Hata hivyo, licha ya nia nzuri ya Serikali ya kufuta riba na adhabu ili kuwawezesha walipa kodi wenye madeni sugu ya kodi kuyalipa kwa awamu ili kurahisisha mwendelezo wa biashara zao, wengi wao hawakulipa kodi hizo hata baada ya kuingia mikataba na TRA na hata baada ya Serikali kuongeza muda wa ziada wa kufanya malipo ya kodi husika yaliyotokana na msamaha huo. (Makofi)