Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 11 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 90 2021-04-16

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mikakati gani wa kumaliza mgogoro kati ya Hifadhi ya Ruaha na Wakulima na Wafugaji wanaozunguka Hifadhi hiyo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Mtega, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali iliunda Kamati iliyojumuisha Mawaziri kutoka Wizara nane kwa ajili ya kufuatilia na kutatua migogoro ya ardhi nchini. Migogoro hiyo iliyofanyiwa kazi na Kamati husika ni pamoja na migogoro kati ya wakulima na wafugaji wanaozunguka Hifadhi ya Taifa Ruaha.

Mheshimiwa Spika, Kamati hiyo imefanya tathmini ya migogoro hiyo na kutoa mapendekezo ambayo yameshatolewa maamuzi na Baraza la Mawaziri kwa ajili ya utekelezaji utakaoanza hivi karibuni.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa rai kwa Mheshimiwa Mbunge pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine na wananchi ambao maeneo yao yana changamoto za migogoro hiyo kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.