Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 26 2020-04-03

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:-

(a) Je, kuna miongozo ya fedha mingapi inayoitaka Halmashauri kutenga fedha za ndani kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo?

(b) Je, ni halali kuwepo miongozo zaidi ya mmoja ukizingatia kuwa sasa Halmashauri hazina ruzuku?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Richard Philip Mbogo, Mbunge wa Nsimbo, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, usimamizi wa fedha kwenye Halmashauri unafanyika kwa kuzingatia Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290. Kifungu cha 37 na Kifungu cha 68 vinampa mamlaka Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa kutoa miongozo ya usimamizi wa fedha katika Serikali za Mitaa.

(b) Mwongozo wa mgawanyo wa mapato ya ndani kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na Matumizi ya Kawaida umezingatia uwezo wa Halmashauri kukusanya mapato ambapo Halmashauri zenye mapato makubwa zinachangia asilimia 60 ya mapato yake kwa ajii ya Miradi ya Maendeleo na Halmashauri zenye mapato kidogo zinachangia asilimia 40 ya mapato yake kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.