Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 46 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 388 2019-06-17

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND (K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA) aliuliza:-

(a) Je, Serikali ipo tayari kuwaeleza Watanzania hususani vijana kuwa hatua gani zimechukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwabaini, kuwachunguza na hatimaye kuwahukumu wale wote waliobainika kujihusisha na mtandao wa biashara za dawa za kulevya?

(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia vijana waliotumbukia kwenye dimbwi la matumizi ya dawa za kulevya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zainab Athuman Katimba, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo;-

Mheshimiwa Naibu Spika, tokea Awamu ya Tano iingie madarakani imewabaini na kuwakamata watuhumiwa kama ambavyo inaorodheshwa hapa chini. Watumiaji wa dawa za kulevya za viwandani mwaka 2016 idadi ya makosa ni 679 na watuhumiwa waliokamatwa ni 1,269 ambao kati ya hao wanaume ni 1,127 na wanawake 142; mwaka 2017 idadi ya makosa ni 902 ambapo watuhumiwa 1,578 walikamatwa kati ya hao 1,485 ni wanaume na 93 ni wanawake; mwaka 2018 makosa yalikuwa ni 702 ambapo watuhumiwa 886 walikamatwa kati ya hao 796 ni wanaume na wanawake walikuwa 90 na mwezi Januari, 2019 hadi Machi, 2019 jumla ya makosa yalikuwa ni 133, watuhumiwa waliokamatwa ni 174 kati ya hao 162 ni wanaume na 12 ni wanawake.

Mheshimiwa Naibu Spika, madawa ya mashambani kwa maana ya mirungi na bangi; mwaka 2016 jumla ya makosa ya madawa ya mashambani ni 10,375 ambapo watuhumiwa walikuwa ni 26,031, kati ya hao wanaume 23,872 na watuhumiwa wanawake walikuwa 2,159; mwaka 2017 makosa ya madawa ya kulevya yalikuwa ni 8,956 na watuhumiwa walikuwa 12,529 wakati wanaume walikuwa 12,529 na wanawake walikuwa ni 1,112; mwaka 2018 makosa yalikuwa ni 7,539 watuhumiwa walikuwa 9,987 ambapo wanaume walikuwa ni 8,935 na wanawake walikuwa ni 1,052 na Januari, 2019 hadi Machi, 2019 makosa yalikuwa 1,842 ambapo wanaume walikuwa 2,340 na wanawake walikuwa 202.

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi watuhumiwa wamepelekwa mahakamani na wengine upelelezi wa kesi zao na mashauri yao unaendelea na uko kwenye hatua tofauti.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi kupitia programu ya kuzuia uhalifu limeendelea kutoa huduma ya urekebishaji kwa waathirika wa dawa za kulevya kwa kutumia vikundi mbalimbali kama vile vya michezo nchini chini ya miradi ya kuzuia uhalifu kama vile familia yangu haina uhalifu na klabu ya usalama kwetu wetu kwanza.