Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 44 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 373 2019-06-12

Name

Munira Mustafa Khatib

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNIRA MUSTAPHA KHATIBU aliuliza:-

Kumekuwa na biashara haramu za mitandao maarufu kama pyramid schemes. Biashara ambazo zimeshamiri sana miji ya Arusha, Dar es Salaam na Mwanza.

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti biashara hizo ambazo zimekuwa na athari kubwa kwa uchumi wa Taifa?

(b) Je, ni kampuni ngapi za aina hiyo ambazo zimeingia nchini na kupata kibali cha kuendesha biashara za aina hiyo?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Munira Mustapha Khatibu, Mbunge wa Viti Maalum, lenye vipengele (a) na (b), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Jinai, Sura Na. 16 kifungu cha 171A, 171B na 171C, biashara ya pyramid schemes au upatu, ni haramu na huendeshwa kinyume na sheria na taratibu za nchi. Ili kudhibiti biashara hiyo, Serikali huchukua hatua dhidi ya wahusika kama ilivyofanya kwa taasisi ya DECI. Aidha, Serikali itaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu ubaya na madhara ya biashara ya upatu. Mathalani tarehe 14 Juni, 2017 Benki Kuu ya Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ilitoa taarifa kwa umma kuhusu madhara ya biashara ya upatu na kuwahimiza wananchi kutoa taarifa kwenye vyombo vinavyohusika pindi wanapopata taarifa ya baadhi ya watu au taasisi kujihusisha na biashara ya upatu.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, biashara ya upatu siyo biashara halali, hivyo hakuna mtu au taasisi yenye leseni ya kufanya biashara hiyo. Kampuni au watu binafsi wanaojihusisha na biashara hiyo wanavunja sheria na wakibainika watachukuliwa hatua za kisheria.