Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Madini 123 2019-09-13

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:-

Je, ni kwa nini mgodi wa GGM umegoma kulipa deni la Halmashauri ya Geita la Dola za Kimarekani 800,000?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Mji wa Geita pamoja na Wilaya ya Geita, kwa pamoja zilikuwa zikidai kiasi cha dola za Kimarekani 800,000, kwa mujibu wa Mkataba wa Maendeleo ya Uwekezaji wa Madini yaani MDA ulioingiwa na Serikali pamoja na Kampuni ya Mgodi ya GGM mwaka 1999. Deni hilo lilitokana na kutokulipwa kwa ushuru wa huduma kiasi cha dola za Kimarekani 200,000 kila mwaka kwa malimbikizo ya miaka minne kuanzia mwaka 2000 - 2003.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Tume ya Madini, ilielekeza Mgodi wa Dhahabu wa Geita kulipa deni hilo kwa Halmashauri ya Mji wa Geita na Halmashauri ya Wilaya ya Geita ili fedha hizo ziweze kuboresha huduma za jamii na za kiuchumi katika Halmashauri hizo. Aidha, tarehe 26 Oktoba, 2018, Mgodi wa Geita Gold Mining ulilipa deni lote lililokuwa likidaiwa kiasi cha Sh.1,814,249,519.99.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchanganuo wa malipo hayo ya ushuru wa huduma yaani service levy ni kiasi cha Sh.1,296,462,706.99 zililipwa kwa Halmashauri ya Mji wa Geita na kiasi cha Sh.517,786,813 zililipwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.