Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 6 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 83 2019-11-12

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-

Miongoni mwa kero za Muungano ni wananchi wa Zanzibar waletapo magari yao Tanzania Bara kutoruhusiwa kutembea mpaka yabadilishwe namba, wakati magari yanayotoka Bara yafikapo Zanzibar yanaruhusiwa kutembea kwa muda wote bila ya bughudha yoyote:-

(a) Je, Serikali inalifahamu suala hili?

(b) Kama ndiyo, je, Serikali ina mpango gani madhubuti wa kutatua suala hili ili Watanzania waendelee kufaidi matunda ya Muungano?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mattar Ali Salum, Mbunge wa Shaurimoyo, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inafahamu kwamba magari yaliyosajiliwa Zanzibar hayaruhusiwi kutembea Tanzania Bara bila kibali maalumu kwa sababu sheria zinazotumika kusajili vyombo vya moto, kati ya pande mbili za Muungano siyo sheria za Muungano. Kwa upande wa Tanzania Bara, usajili wa vyombo vya moto unasimamiwa na Sheria ya Usalama Barabarani ya mwaka 1973 pamoja na Kanuni zake na kwa upande wa Zanzibar usajili wa vyombo vya moto unafanyika kwa mujibu wa Sheria ya Usafiri wa Barabara Na.7 ya mwaka 2003. Aidha, majukumu ya usajili wa vyombo vya moto kwa upande wa Zanzibar husimamiwa na Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) na Tanzania Bara husimamiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuondokana na utaratibu wa sasa wa wananchi wa Zanzibar kuomba kibali maalum ili kutembelea magari yao Tanzania Bara, Serikali za pande mbili zipo katika majadiliano ili kuhuisha sheria na mifumo ya ukukotoaji kodi ya magari na hivyo kuwawezesha wananchi kutembelea magari yao pande zote za Muungano bila usumbufu. Aidha, mchakato wa kuhuisha sheria na mifumo ya ukokotoaji kodi utafuata taratibu zote zilizowekwa na Bunge lako Tukufu pamoja na Baraza la Wawakilishi Zanzibar.