Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 72 2019-11-12

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:-

Wananchi wa Mipande – Mtengula na Mwitika Maparawe wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa madaraja na Rais wa Awamu ya Tano aliwaahidi Wananchi hao kuwajengea madaraja:-

Je, ni lini ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerome Dismas Bwanausi, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) imeanza usanifu wa Daraja la Mwitika hadi Maparawe linalounganisha barabara yenye urefu wa kilomita 4 na daraja la Mputeni-Mtengula linalounganisha barabara yenye urefu wa kilomita 3.06. Lengo la usanifu huo ni kubaini gharama zinazohitajika kwa ajili ya ujenzi wa madaraja yote mawili. Hivyo, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira wakati Serikali inakamilisha kazi hiyo ya usanifu ili kuanza shughuli za ujenzi.