Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 39 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 323 2018-05-29

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kukipatia Kituo cha Chanika gari la patrol?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikabe Waitara, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kipolisi ya Ukonga ipo katika Mkoa wa Kipolisi Ilala na Kituo Kikuu ni Kituo cha Polisi Stakishari ambacho kinasaidiwa na vituo vingine vidogo kama vile Pugu, Chanika, Msongola, Gongolamboto, Mazizini, Karakata, Kinyerezi, Tembo Mgwaza na Kitunda. Vituo hivi vyote huhudumiwa kwa magari saba toka katika Kituo cha Stakishari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha katika Kituo cha Polisi cha Chanika lipo gari Na. PT 1889 Toyota Land Cruiser Pickup, ndilo hutumika kufanya doria katika eneo hilo likisaidiwa na magari mengine toka katika Kituo cha Stakishari, kwani kituo hiki ni kikubwa ukilinganisha na vituo vingine vilivyotajwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi litaangalia uwezekano wa kuongeza gari katika Kituo cha Polisi Chanika na kuzingatia vigezo kama vile hali ya uhalifu, idadi ya watu, sababu za kiutawala na kijiografia kwa kulinganisha na maeneo mengine yenye mahitaji kama haya.