Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2018-02-02

Name

Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:-
Zahanati ya Kalenga iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa haikidhi mahitaji halisi ya wakazi wa vijiji vinavyoizunguka.
Je, ni lini Serikali itaboresha zahanati hiyo kwa kujenga vyumba vya ziada na mahitaji mengine ya msingi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zainabu Nuhu Mwamwindi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Zahanati ya Kalenga ilijengwa zaidi ya miaka 40 iliyopita. Kutokana na ongezeko la watu, kwa sasa zahanati hii imekuwa ikitoa huduma kwa wananchi ambao wamekuwa wengi kuliko ilivyokuwa hapo awali. Hata hivyo, Halmashauri haiwezi kuongeza majengo kwenye eneo la zahanati hii, kwani tayari imezungukwa na makazi ya watu, hivyo hakuna nafasi ya kuongeza majengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto hiyo, baadhi ya vijiji vilivyokuwa vinapata huduma kwenye zahanati hii, vimejengewa zahanati ambayo ni zahanati ya Mangalali iliyofunguliwa mwezi Februari, 2017. Zahanati hii imesaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika zahanati ya Kalenga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, juhudi zinafanyika kwa kuhamasisha ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kata ya Jirani ya Mlanda. Ujenzi huu unafanyika kwa nguvu za wananchi na upo katika hatua za awali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri katika mpango wa bajeti wa mwaka 2018/2019 imetenga kiasi cha shilingi milioni 54 ili kufanikisha ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kata ya Mlanda. Kituo hicho kitakapokamilika, kwa kiasi kikubwa kitapunguza msongamano wa wagonjwa katika Zahanati ya Kalenga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kuziagiza Halmashauri zote nchini kutenga maeneo ya kutosha kwa ajili ya Taasisi za Umma kama vile shule, vituo vya kutolea huduma za afya na Ofisi za Vijiji, Mitaa, Kata na kuhakikisha maeneo haya yanapimwa na kupatiwa Hati Miliki ili kuondoa changamoto zinazoweza kujitokeza siku za usoni.