Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 10 2018-01-30

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itakamilisha miradi ya umeme katika vijiji ambavyo havijafikiwa katika Halmashauri ya Momba?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ni kufikisha umeme katika vijiji vyote visivyo na umeme nchini ikiwemo vijiji vya Wilaya ya Momba ifikapo Juni, 2021. Katika Wilaya ya Momba jumla ya vijiji 27 vitapatiwa umeme kupitia mzunguko wa kwanza wa awamu ya tatu ya miradi ya kusambaza umeme vijijini. Vijiji hivyo ni pamoja na Ikana, Nakawale, Ipanga, Mpui, Mfuto, Machindo, Muungano, Samang’ombe, Tundumakati, Unyamwanga, Nello, Tukuyu, Mlimani, Majengo Mapya, Ihanda na Migombani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za mradi zinazotekelezwa na Kampuni ya STEG International ambazo zinahusisha ujenzi wa kilometa 60 za umeme msongo wa kilovoti 33 na kilometa 108 za njia za umeme msongo kilovoti, kufunga transfoma 54 na kuunganisha wateja 1,773. Gharama ya mradi inakadiriwa kuwa shilingi 6,607,000,000 na mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Aprili, 2019.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vitakavyobakia katika mzunguko wa kwanza wa REA III vitapatiwa umeme katika mzunguko wa pili wa REA-III iunaotarajiwa kuanza mwezi Aprili, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021.