Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2024-01-30

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:-

Je, zabuni ngapi zilitolewa na Halmashauri za Majiji, Manispaa na Wilaya kwa makundi maalum hasa wanawake kama sheria inavyotaka?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2011 na Marekebisho yake ya mwaka 2016 katika Kifungu cha 64 (2) (c) na Tangazo la Serikali Na. 333 la Mwaka 2016, taasisi zinapaswa kutenga asilimia 30 ya manunuzi kwa ajili ya makundi maalum.

Mheshimiwa Spika, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimeweka utaratibu wa kusajili Makundi Maalum ya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu. Aidha, vikundi maalum vipatavyo 345 vimesajiliwa katika Halmashauri ambavyo vimekidhi vigezo vya kupewa zabuni. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, jumla ya vikundi 228 vya makundi maalum vilipewa zabuni mbalimbali katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ikiwa ni sawa na asilimia 66. Aidha, kati ya hivyo, vikundi vya wanawake vipatavyo 70 vilipata zabuni.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutoa elimu kwa watendaji ngazi ya Halmashauri ili kuweza kusimamia na kuwahamasisha wananchi wenye sifa kujiunga na vikundi kwa ajili ya kupata fursa za zabuni kadri ya sheria zilizopo, ahsante