Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 51 2024-02-02

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko la kisasa Holili Wilayani Rombo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuena Athumani Bushiri, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na Soko la kisasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Rombo eneo la Holili. Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023 ilitenga na kutoa shilingi milioni 75 fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya ujenzi wa vyoo na kumwaga jamvi eneo la kuuzia mazao.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu kwa ajili ya kujenga na kuendeleza miundombinu inayohitajika ili kuwezesha soko hilo kuwa la kisasa na kukidhi mahitaji, ahsante.