Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 27 2024-04-03

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO aliuliza: -

Je, lini Bima ya Afya kwa watu wote itaanza kutumika?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Furaha Ntengo Matondo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ilipitishwa na Bunge tarehe 1 Novemba, 2023 na Mheshimiwa Rais ameidhinisha sheria hiyo tarehe 19 Novemba, 2023 na imechapishwa katika gazeti la Serikali la tarehe 1 Desemba, 2023.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza maandalizi ya kuanza kutumika kwa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ambapo kwa mujibu wa Kifungu cha kwanza cha Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote Waziri anaweza kuteua baadhi ya vifungu vya kuanza kutumika. Baadhi ya vifungu ambavyo vinaweka mifumo imara ya kutekeleza Bima ya Afya kwa Wote vimeainishwa na kuwasilishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Sheria itatangazwa kuanza kutumika kabla ya mwisho wa mwezi wa Aprili, 2024 kwa tarehe itakayotajwa.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.