Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 2 Planning and Investment Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji 21 2024-04-03

Name

Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Primary Question

MHE. TOUFIQ SALIM TURKY aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga majengo ya viwanda kuwapangishia wawekezaji wazawa ili kuongeza idadi kwani gharama za kuanzisha kiwanda ziko juu?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, mwelekeo wa Sera za Serikali katika uwekezaji ni kushirikiana kati ya sekta ya umma na sekta binafsi katika maendeleo ya viwanda. Serikali ina jukumu la msingi la kutwaa, kupima na kupanga matumizi ya ardhi, wakati sekta binafsi hukaribishwa na kuhamasishwa kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu ya viwanda. Utaratibu huu umeshaanza kuzaa matunda ambapo hadi kufikia Desemba jumla ya kongani kubwa tatu za viwanda zimejengwa kwa ushirikiano kati ya sekta binafsi na Serikali.