Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 18 2024-04-03

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je, lini Serikali itakarabati shule chakavu za msingi katika Jimbo la Lushoto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Jimbo la Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kufanya ukarabati wa shule chakavu nchini ikiwemo zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ambapo katika Mwaka wa Fedha 2022/2023, Serikali imetoa shilingi milioni 796.5 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa Shule ya Msingi Mshangai na Kwemshai katika Jimbo la Lushoto.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2023/2024, Serikali imetoa shilingi milioni 180 kwa ajili ya ukarabati wa Shule Kongwe nne za Nyankei, Mhelo, Hemtoye na Mbaramo. Ahsante.