Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 17 2024-04-03

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI K. NDINGO aliuliza: -

Je, lini Serikali itakarabati shule kongwe za msingi zilizopo Mbarali ambazo zipo katika hali mbaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bahati Keneth Ndingo, Mbunge Wa Jimbo la Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya elimu ikiwemo ujenzi wa madarasa mapya na ukarabati wa madarasa chakavu. Katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 na 2023/2024, Serikali imetumia shilingi milioni 360 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa madarasa 18 mapya katika Shule Kongwe za Chimala, Igalako, Ujewa na Isitu.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2024/2025, Serikali imetenga shilingi milioni 180 kwa ajili ya ukarabati wa shule kongwe za Ipwani, Ibumila na Mbuyuni. Aidha, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ukarabati wa shule kongwe kote nchini. Ahsante.