Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 16 2024-04-03

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:-

Je, nini mkakati wa Serikali kuajiri wasaidizi kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wenye ulemavu uliozidi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stela Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuwahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum kunahitaji kada ya wasaidizi wenye taaluma ya kutoa usaidizi kwa wanafunzi hao kulingana na changamoto zinazowakabili, ikiwa ni pamoja na kuwapa msaada wa awali pale inapohitajika. Kwa sasa Serikali imeendelea kuwatumia Walimu, wataalam waliosomea elimu maalum kuwafundisha na kuwahudumia wanafunzi hao.

Mheshimiwa Spika, pindi kada saidizi kitaalam kwa wanafunzi wenye ulemavu itakapotambulika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI iko tayari kutoa ushauri wa kuajiri ili waweze kutoa usaidizi wa kitaalam kwa wanafunzi wenye changamoto kubwa zaidi. Ahsante.