Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 106 2023-11-07

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -

Je, wakandarasi wangapi kutoka Mkoa wa Kagera wamepata kazi katika mnyororo wa ujenzi wa Bomba la Mafuta la Hoima – Tanga?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakandarasi Wakuu wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta kutoka Hoima (Uganda) hadi Chongoleani (Tanga) wameendelea kushirikiana na Wakandarasi wadogo wajenzi pamoja na watoa huduma mbalimbali katika maeneo yote inayopitiwa na mradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Mkoa wa Kagera hadi sasa, jumla ya wakandarasi na watoa huduma 42 wamepatiwa kazi mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa ujenzi wa mradi huu, zikiwemo uuzaji wa vifaa vya ujenzi, huduma za usafirishaji, ulinzi, usambazaji wa mafuta, huduma za umeme na hoteli, nashukuru.