Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Finance Wizara ya Fedha 103 2023-11-07

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kutenganisha malipo ya majengo kwa nyumba yenye zaidi ya mita moja ya umeme?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing'oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha ukusanyaji wa mapato kupitia mfumo wa luku kwa nyumba ambayo ina mita zaidi ya moja kwa kuhakikisha inalipiwa mita moja pekee. Aidha, pale inapobainika majengo mawili au zaidi kutumia mita moja tumekuwa tukifanya maboresho ya utozaji kwa kutoza kiasi kinachopaswa kutozwa kwa kila jengo kwa mita iliyopo. Lengo la hatua hii ni kuhakikisha msingi wa utozaji wa kodi ya majengo unazingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kutokana na malalamiko ya majengo machache kujitokeza kwa uchache katika kusajili na kutoa taarifa sahihi za majengo yao, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) iliendelea na zoezi la uhakiki kwa kutumia vyanzo kutoka Mamlaka mbalimbali za Serikali. Aidha, TRA inaendelea na maboresho ya taarifa za wamiliki wa majengo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie Bunge lako Tukufu kwa kuwataka wamiliki wote wa majengo ambao watakuwa na changamoto za ulipaji kodi ya majengo kupitia ununuzi wa umeme ikiwa ni pamoja na uwepo wa mita zaidi ya moja katika jengo moja, kufika katika Ofisi za Malamka ya Mapato Tanzania iliyokaribu nao kwa ajili ya kufanya maboresho ya taarifa.