Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 99 2023-11-07

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-

Je, lini Kata za Ruvu, Msindo, Mshewa, Vudee, Mhezi, Tae na Suji - Same zitapelekewa mawasiliano ya simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Jimbo la Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeainisha Kata Sita kati ya Kata Saba za Jimbo la Same Magharibi zenye changamoto kubwa ya upatikanaji wa huduma za Mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata za Vudee, Suji na Ruvu zitafikishiwa huduma ya mawasiliano kwa kupitia Kampuni ya Horora PLC (TiGo), wakati Kata ya Mshewa itafikishiwa huduma za mawasiliano kupitia kampuni ya simu ya Airtel. Kata ya Msindo itafikishiwa huduma za mawasiliano na kampuni ya simu ya TTCL na Kata ya Mhezi itafikishiwa huduma ya mawasiliano ya simu kupitia kampuni ya simu ya Halotel.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Kata ya Tae, USCAF itaifanyia tathmini Kata hiyo ili kubaini mahitaji halisi ya huduma za mawasiliano na hatimae kuiweka katika mpango wa zabuni zijazo zitakazotekelezwa kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.