Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 98 2023-11-07

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itarudisha masomo ya kazi za mikono kama useremala, mapishi, kushona, kilimo, ujenzi kwa shule za Msingi na Sekondari?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha taratibu za kufanya mapitio na kuboresha mitaala ya ngazi ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Elimu ya Ualimu. Katika maboresho hayo, fani za ufundi zaidi ya 55 zikiwemo useremala, mapishi, kushona, kilimo na ujenzi zimejumuishwa katika mitaala mipya. Hivyo, wanafunzi watapata fursa ya kujifunza kazi za mikono kupitia chaguzi za mikondo ya masomo kwa kadri ya amali watakazozipenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mafunzo haya katika ngazi ya Sekondari yatatolewa kwa kutumia mtaala wa VETA na yatatahiniwa na NACTVET kwa lengo la kuwezesha wahitimu kupata vyeti vitakavyotambulika katika soko la ajira,. Nakushukuru.