Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 95 2023-11-07

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa fedha zote za ujenzi wa barabara ya lami Karatu – Mbulu – Hydom hadi Sibiti ili ujenzi uendelee?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti – Lalago mpaka Maswa yenye urefu wa kilometa 389 inatekelezwa kwa kutumia fedha za ndani na kwa utaratibu wa EPC+F. Awamu ya kwanza: Mbulu – Garbabi (kilomita 25) Mkandarasi yupo eneo la mradi anaendelea na kazi. Eneo la Labay – Haydom (kilomita 25) Mkandarasi anakamilisha taratibu za kimkataba ili aweze kulipwa Malipo ya Awali (Advance Payment) ili aweze kuanza kazi. Sehemu iliyobaki ya Karatu – Mbulu na Haydom – Sibiti – Lalago – Maswa yenye urefu wa kilomita 339 itajengwa kwa utaratibu wa EPC+F ambapo Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 16 Juni, 2023, ahsante.