Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 91 2023-11-07

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, ni nini Mpango wa Serikali kudhibiti Mto Nakasangwe na Mto Tegeta na kadhalika inayopanuka kwa kasi na kutishia maisha ya watu na mali katika Jimbo la Kawe?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Jimbo la Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imechukua hatua mbalimbali kukabiliana na changamoto za kupanuka kwa Mto Nakasangwe na Mto Tegeta kama ifuatavyo:

i. Kuandaa Mwongozo wa usafishaji mchanga, tope na taka ngumu kwenye mito na mabonde kwa Mkoa wa Dar es Salaam.

ii. Kutoa elimu kupitia vipindi vya redio, televisheni, maonesho na mikutano kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa vyanzo vya maji katika ngazi zote ili kuongeza kasi ya uhifadhi vya vyanzo vya maji na kingo za mito.

iii. Kuhamasisha Umma kuhusu upandaji wa miti rafiki kwa vyanzo vya maji ambavyo itasaidia katika kuzuia mmomonyoko wa kingo za mito na kuimarisha mtiririko wa maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kusisitiza utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Sura 191 kuhusu uhifadhi ya eneo la mita 60 katika kingo za mito, fukwe za bahari na maziwa yanayozuia matumizi yeyote ya kibinadamu katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa kutambua kupanuka kwa kingo za mto Tegeta na Nakasangwe, Serikali itaangalia uwezekano wa kufanya tathmini katika maeneo hayo kwa lengo la kupata suluhisho la kudumu kama ilivyofanyika katika maeneo mengine ambapo Serikali ilibuni na kutekeleza miradi ya ujenzi wa kuta, kama vile ujenzi wa ukuta wa Pangani na fukwe katika Barabara ya Barak Obama katika jiji la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.