Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 12 2023-11-01

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italeta Sheria ya kuruhusu halmashauri kutumia benki kama wakala wa ukopeshaji na ukusanyaji madeni?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Yahya Mhata, Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua ufanisi wa kutumia benki kama wakala wa ukopeshaji na ukusanyaji wa mmadeni kwa kuzingatia kuwa benki zina miundombinu na utaalamu wa kutoa huduma hizo. Hata hivyo, ili kutumia benki katika kutekeleza jukumu la mikopo ya asilimia 10, maandalizi na utafiti unapaswa kufanyika ili kuendana na lengo kusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, iliunda Kamati ya Kitaifa ambayo ilichambua na kuandaa mapendekezo ya uendeshaji wa mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. Aidha, timu imeshakamilisha kazi hiyo na kuwasilisha maoni na mapendekezo ambapo Serikali inaendeleia kuifanyia kazi na baada ya kukamilisha itatoa utaratibu, ahsante.