Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 126 2024-02-07

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO K.n.y. MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, ni malambo/mabwawa mangapi yatajengwa katika Halmashauri ya Itigi kwa ajili ya kunyweshea Mifugo?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua changamoto ya upatikanaji wa maji kwa ajili ya mifugo katika maeneo mbalimbali hapa nchini, ikiwemo katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi. Aidha, mwaka 2021/2022 Serikali ilikamilisha ujenzi wa bwawa la kunyweshea mifugo katika Kijiji cha Mhanga Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mahitaji ya mabwawa na visima kwa ajili ya maji ya mifugo nchini ni makubwa. Hivyo, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ujenzi wa mabwawa na kuchimba visima katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi. Kulingana na upatikanaji wa fedha, vilevile, ili kukabiliana na upungufu uliopo, na nitoe wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kuhamasisha wafugaji na wadau wengine kuwekeza katika miundombinu ya maji ya mifugo.