Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 123 2024-02-07

Name

Abdi Hija Mkasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza:-

Je, lini Kituo cha Polisi Micheweni kitakarabatiwa ili kiendane na hadhi ya Wilaya?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdi Hija Mkasha, Mbunge wa Micheweni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi ilifanya tathmini kwa ajili ya kubaini kiwango cha uchakavu na gharama za ukarabati wa jengo la Kituo cha Polisi Micheweni na kubaini kuwa jumla ya shilingi milioni 65 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati huo. Fedha hizo zimetengwa kupitia Mfuko wa Tuzo na Tozo katika mwaka wa fedha 2023/2024. Mara fedha hizo zitakapopokelewa, zitatumwa katika kituo hicho ili ukarabati wake uanze kufanyika, nashukuru.